SOKA: Mourinho “Hazard nifuate Roma”
2021-05-27 17:09:46| cri

Kocha wa Roma, Jose Mourinho, anataka kumsajili staa wa Real Madrid aliyewahi kufanya naye kazi Chelsea, Eden Hazard. Wawili hao walikuwa pamoja wakati Mourinho aliporejea Stamford Bridge kuanzia mwaka 2013 hadi 2015. Hazard anapitia wakati mgumu Madrid tangu ajiunge nayo akitokea Chelsea mwaka 2019, sababu kubwa ikiwa ni majeraha. Kwa miaka zaidi ya miwili aliyokaa Madrid, Mbelgiji huyo amecheza mechi 43 tu, akifunga mabao matano na kutoa ‘asisti’ nane.