Mwaka huu ni maadhimisho ya miaka 100 tangu kuanzishwa kwa Chama cha Kikomunisti cha China. Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China imeamua kutoa “medali ya tarehe Mosi, Julai” kwa mara ya kwanza, ili kuwapongeza wanachama hodari wa chama hicho waliotoa mchango mkubwa kwa wananchi.
Medali hiyo ni heshima ya juu zaidi katika Chama cha Kikomunisti cha China, ambayo inajumuisha nembo ya chama, nyota yenye alama tano, bendera, mnara na nuru, alizeti, mlima na mto, na wingu.