• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (21 Oktoba-27 Oktoba)

    (GMT+08:00) 2017-10-27 18:17:15
    Rais wa Catalonia afuta nia yake ya kuitisha uchaguzi wa haraka

    Rais wa Catalonia Carles Puigdemont ambaye siku ya Alhamisi alitarajiwa kuhutubia wananchi wa eneo hilo kuhusu kuitisha uchaguzi wa haraka wa uhuru wa jimbo hilo ameamua kuachana na uwezekano huo.

    Uongozi wa jimbo la Catalonia nchini Uhispania, ulitarajiwa kutisha Uchaguzi mpya wa wabunge wa jimbo hilo.

    Uchauzi huo ulikua unatarajiwa kufanyika tarehe 20 mwezi Desemba, na ungelilenga kuhakikisha kuwa jimbo hilo linajitenga kabisa na Uhispania.

    Aidha, uongozi huo unatarajiwa kutoa tangazo la eneo hilo kujitenga, hatua ambazo zinapingwa vikali na serikali ya Madrid.

    Mapema wiki hii Uhispania ilitangaza kwamba itachukua hatua za kufutilia mbali utawala wa Catalonia ikiwa kiongozi wake hataachana na hatua za kutafua uhuru, naibu waziri mkuu amesema.

    Soraya Sáenz de Santamaría alitoa onyo siku moja moja kabla ya siku aliyopewa Carles Puigdemont, kumalizika.

    Serikali ya Catalonia imesisitiza kuwa haiwezi kutekeleza matakwa ya Madrid baada ya kura iliyokumbwa na utata ya Catalonia.

    Kumekuwa na maandamano kupinga kuzuiwa kwa viongozi wa vugugu la Catalonia.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako