Rais Xi aongoza mafunzo ya 31 ya pamoja ya ofisi ya siasa ya kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha China
2021-06-27 12:35:38| CRI

Rais Xi aongoza mafunzo ya 31 ya pamoja ya ofisi ya siasa ya kamati kuu ya chama cha kikomunisti cha China_fororder_图像_2021-06-28_121941

Ofisi ya siasa ya kamati kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China CPC imefanya mafunzo ya 31 ya pamoja. Mafunzo hayo yamefanywa kwa mtindo wa matembezi na mjadala. Viongozi wa chama na serikali akiwemo Xi Jinping, Li Keqiang, Li Zhanshu, Wang Yang, Wang Huning, Zhao Leji na Hanzheng wametembelea makazi ya zamani ya rais wa zamani wa China Marehemu Mao Zedong.