Maonesho ya 17 ya Kimataifa ya Katuni kuwavutia watu wengi
2021-09-28 14:38:28| Cri

Viwanda elfu 17 kutoka ndani na nje ya China vitashiriki kwenye Maonesho ya 17 ya Kimataifa ya viwanda vya katuni ya China yatakayofanyika kuanzia Septemba 29 hadi Oktoba 4 mjini Hangzhou, nchini China.

Maonesho hayo yatakayovutia watu wengi, yatafanyika kwa kutumia sayansi na teknolojia mpya zikiwemo teknolojia ya 5G na data kubwa.