Lugha ya Kichina na Kiswahili zinavyobadili maisha ya wanawake wa China na Afrika Mashariki
2021-11-03 10:34:11| Cri

 

Lugha ya Kichina na Kiswahili zinavyobadili maisha ya wanawake wa China na Afrika Mashariki_fororder_Wanjala 图片

Lugha kama chombo cha mawasiliano hutumika kama daraja baina ya jamii na jamii nchi na nchi au hata bara na bara. Lugha za Kiswahili na Kichina kwa sasa zimeleta manufaa kwa wazungumzaji wa pande zote mbili, na wengi wao sasa wamekuwa na ari na hamu ya kutaka kujifunza lugha hizi kwani zinawasaidia katika biashara zao, shughuli za utamaduni au hata mawasiliano wakati wanapotembeleana.