WHO: Marufuku ya usafiri haiwezi kuzuia kuenea kwa virusi vya aina ya Omicron
2021-12-01 09:00:34| cri

WHO: Marufuku ya usafiri haiwezi kuzuia kuenea kwa virusi vya aina ya Omicron_fororder_VCG111359425664

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema, marufuku kamili ya usafiri haitazuia kuenea  kwa aina mpya ya virusi vya Omicron kimataifa, na itakuwa mzigo mkubwa kwa maisha ya watu.

Taarifa iliyotolewa na Shirika hilo imesema, jumapili iliyopita Shirika hilo liliorodhesha virusi hivyo kama virusi vinavyohitaji kufuatiliwa, na tangu wakati huo, nchi nyingi zimeweka vikwazo vya muda vya kusafiri, ikiwa ni pamoja na kupiga marufuku wasafiri kutoka nchi za kusini mwa Afrika, na kuzuia wasafiri kutoka nchi zilizogundulika kuwa na virusi hivyo.