Watu 17 wafariki katika ajali ya treni nchini Iran
2022-06-09 08:45:23| cri

Watu 17 wamefariki katika ajali ya treni ya abiria jana nchini Iran.

Shirika la Reli la Iran limesema, treni iliyokuwa na abiria 430 iligongana na mashine ya kuchimba na kuacha njia na kusababisha uharibifu wa mabehewa sita. Kazi ya uokoaji bado inaendelea.