Rais anayemaliza muda wake nchini Kenya Uhuru Kenyatta alifanya mkutano jana Jumatatu na mrithi wake William Ruto, akisisitiza nia yake ya kupokezana madaraka kwa amani nchini humo.
Kenyatta, ambaye baada ya mkutano wake na Ruto katika ikulu jijini Nairobi, alilihutubia taifa akitoa mkono wa kwaheri kupitia televisheni akisema atasimamia mchakato wa kupokezana madaraka leo Jumanne ili kuthibitisha tena upevu wa demokrasia nchini Kenya. Aidha Kenyatta alimpongeza Naibu wake Williamu Ruto kwa kushinda kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Agosti 9 na kutoa wito wa kuunga mkono serikali ijayo ambayo imedhamiria kuhudumia wananchi wote kwa usawa.
Katika hafla ya kuapishwa itakayofanyika leo, Kenyatta atamkabidhi Ruto alama za madaraka zikiwemo upanga na nakala ya katiba kuashiria mapokezano ya madaraka.