Wizara ya ulinzi wa raia ya Mexico imesema, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.7 kwenye kipimo cha Richter lililotokea katika jimbo la Michoacán limesababisha vifo vya watu wawili na wengine 10 kujeruhiwa.
Gavana wa jimbo hilo Bw. Alfredo Ramirez Bedoría amesema, zaidi ya nyumba 3,000 na hospitali 20 ziliharibiwa katika tetemeko la ardhi, ambalo pia lilisababisha maporomoko ya ardhi yaliyoziba baadhi ya barabara. Amesema kazi ya kusafisha barabara hizo bado inaendelea.