Nchi za Afrika zahimizwa kuhusisha uendelezaji wa viwanda na biashara huria ya bara zima
2022-10-21 09:33:18| CRI

Umoja wa Afrika umetoa wito kwa nchi za Afrika kuimarisha kwa pamoja Mkataba wa Eneo la Biashara Huria la Bara la Afrika (AfCFTA) na uendelezaji wa viwanda katika bara hilo ili kutimiza matarajio muhimu ya maendeleo ya Afrika.

Umoja wa Afrika umesema katika taarifa yake kuwa, kuendeleza AfCFTA sambamba na ukuaji wa viwanda kwa juhudi za pamoja ili kutimiza mategemeano yanayohimizana kati ya hizo mbili, ni nguzo muhimu ya mafanikio ya Afrika na Ajenda ya 2063.

Kauli hiyo imetolewa kabla ya mkutano wa Umoja wa Afrika kuhusu Uendelezaji wa Viwanda na Anuwai ya Uchumi, unaotarajiwa kufanyika Novemba 20-25 huko Niamey, mji mkuu wa Niger.