Watu 287 wauawa katika mapambano ya kikabila katika Jimbo la Blue Nile nchini Sudan
2022-10-31 08:49:15| cri

Waziri wa Afya wa Jimbo la Blue Nile Bw. Jamal Nasir amesema, jumla ya watu 287 waliuawa na wengine 239 kujeruhiwa katika mapigano ya hivi karibuni ya kikabila katika jimbo hilo lililoko kusini mashariki mwa Sudan.

Bw. Nasir pia alisema idadi ya waathiriwa itaendelea kuongezeka. Timu za madaktari wa kuchunguza maiti wanatarajiwa kutoa sababu za vifo vya watu walioteketea kwa moto ili kugundua kama walishambuliwa kwa silaha au kupigwa.