Mbinu zinafuata maumbile
2022-11-14 11:14:54| CRI

Zaidi ya miaka 2,700 iliyopita, mwanzilishi wa falsafa ya Dini ya Kitao Lao Tzu aliweka mbele kwamba "Mbinu zinafuata maumbile", ikimaanisha kuwa uendeshaji wa vitu na viumbe vyote ulimwenguni lazima ufuate sheria za maumbile. Binadamu na mazingira ya asili haviwezi kutenganishwa, na falsafa ya "masikilizano kati ya binadamu na mazingira ya asili" ni sehemu kuu ya utamaduni wa jadi wa Kichina.