Kenya yasema watu milioni 4.3 wana uhaba wa chakula kutokana na ukame mkali
2022-11-15 10:13:58| CRI

Mamlaka ya Kudhibiti Ukame ya Kitaifa ya Kenya (NDMA) imesema katika chapisho lake jipya lililotolewa jana Jumatatu kwamba idadi ya Wakenya wanaokabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula imefikia milioni 4.35, na msimu mfupi wa mvua wa Oktoba hadi Desemba unakatisha matumaini ya mavuno mengi katika maeneo mengi ya nchi hiyo.

Kwa mujibu wa NDMA, watoto 942,000 wenye umri wa miezi sita hadi 59 pamoja na akina mama 134,000 wanaonyonyesha katika kaunti zaidi ya 20 zilizoathiriwa na ukame au nusu kame wana utapiamlo na wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.

Kenya inakabiliwa na uhaba mkubwa zaidi wa chakula katika miongo minne iliyopita kufuatia misimu minne mfululizo ya uhaba wa mvua,  athari mbaya za janga la COVID-19, pamoja na gharama kubwa ya mafuta na pembejeo za shambani kama mbolea.

Rais wa Kenya William Ruto amesisitiza dhamira ya serikali ya kuwekeza katika miradi ya kuhimili uhaba wa mvua kama vile kilimo cha umwagiliaji, kupitishwa kwa aina bora za mazao, na ufugaji unaozingatia hali ya hewa ili kusaidia kupunguza njaa na utapiamlo nchini humo.