Mkuu wa CMG atoa salamu za mwaka mpya
2022-01-01 15:18:58| cri

Mkuu wa CMG atoa salamu za mwaka mpya_fororder_图像_2022-01-01_151840

Marafiki wapendwa:

Mwanga wa kwanza wa jua wamwaka mpya unafika duniani. Mwaka mpya ni mwaka wa chui milia kwa kalenda ya kilimo ya China. Kutoka Beijing nawatakia heri ya mwaka mpya na muwe na nguvu kama chui milia!

Mwaka 2021, China iliadhimisha miaka 100 tangu chama cha kikomunisti cha China kianzishwe. Kutoka wanachama zaidi 50 wa miaka 100 iliyopita hadi sasa kuwa na wanachama zaidi milioni 90, chama cha kikomunisti cha China kimeongoza watu wa China kupata mafanikio makubwa. Kuingia zama mpya, chini ya uongozi wa rais Xi Jinping wa China, nchi yetu yenye watu bilioni 1.4 imetimiza lengo la kujenga jamii yenye maisha bora, na kutatua suala la umaskini uliokithiri lililosumbua taifa la China kwa maelfu ya miaka. Kituo kikuu cha redio na televisheni cha China CMG kimeandaa vipindi mbalimbali kama vile “Kuijenga China mpya”, “Kutokomeza Umaskini”, “Maisha bora ya wananchi”, ili kuweka kumbukumbu za zama zetu, na kuweka kumbukumbu za juhudi za chama cha kikomunisti cha China na wananchi wa China, na kimetoa maelezo kwa jumuiya ya kimataifa kuhusu “chanzo cha ndani” cha kuwezesha chama cha kikomunisti cha China kudumisha nguvu zake . Mwezi mmoja uliopita, wakati wa kuadhimisha miaka 80 tangu matangazo ya radio ya China kwa nchi za nje yaanzishwe, rais Xi Jinping alituma barua ya pongezi kwa kituo chetu, kututia moyo kueleza vizuri mambo kuhusu China, kutoa sauti ya China, kujenga vyombo vya habari vya aina mpya vyenye nguvu ya kuongoza , nguvu ya uenezi na ushawishi duniani. Sisi tutaendelea kufanya juhudi kusonga mbele kwa ajili ya kutimiza lengo hilo.

Wahenga wa China wanasema, “taabu na umaskini vinasaidia kuleta mafanikio”. Kutokana na mabadiliko yaliyotokea katika miaka 100 na maambukizi ya COVID-19, dunia ya sasa haijatulia, lakini hatua zetu za kujipatia amani, maendeleo na furaha hazijasimama. Vipindi vyetu vya “China katika Hadithi”, “China kwenye Vitabu”, “Majina ya sehemu za China” na kadhalika vinashuhudia historia ndefu yenye mambo mengi makubwa ya China na maisha mazuri na halisi ya watu wa China. Vipindi vya “Bustani za Taifa”, “Olimpiki kwenye sanaa” na kadhalika, vinaleta sura ya kuvutia ya “China yenye mandhari nzuri” na “China yenye maendeleo ya sekta ya afya” katika zama mpya. Na matangazo ya moja kwa moja ya “darasa kwenye anga ya juu” katika kituo cha China kwenye anga ya juu yameng’arisha ndoto za watoto wengi za kutafiti maajabu ya ulimwengu. Katika tukio kuhusu Ndovu 16 wa Yunnan waliohama kwa muda wa zaidi ya nusu mwaka, vyombo vipya vya habari vya CGTN, CMG Mobile na CCTV NEWS vilifuatilia na kurusha matangazo ya moja kwa moja ya video kwa zaidi ya saa 7000, hali ambayo ilileta ufuatiliaji mkubwa wa watazamaji.

Kutegemea hali halisi ni kanuni ya kimsingi ya wanahabari wa kote duniani. Katika mwaka uliopita, tulishikilia kueleza ukweli wa mambo kwa kutetea haki na usawa. Kukabiliana na “orodha ya mapambano dhidi ya COVID-19 duniani” isiyo ya kweli, tuliandaa “hojaji ya uchunguzi wa maoni ya watumiaji wa mtandao wa Internet duniani” mara tatu, kueleza ukweli wa mambo, kubainisha usahihi na makosa, na kupata majibu na kukubaliwa na mamia ya mamilioni ya watumiaji wa mtandao wa Internet katika nchi mbalimbali. Kuhusu hali ya Afghanistan, video zilizotolewa na waandishi wa habari wa CMG zilifichua ukweli wa baadhi ya nchi kutumia vibaya nguvu na kupuuza maisha ya watu, ambazo zimechukuliwa na vyombo vya habari vya kimataifa kuwa vyanzo muhimu vya habari vya kuaminika . Tutaendelea kufuata kanuni za kazi za vyombo vya habari vya kuwajibika, kufanya juhudi katika kutafuta ukweli na kufichua hali halisi! Tunatumai wenzetu wa nchi za magharibi wathamini pamoja nasi sifa ya vyombo vya habari! Tuache ukweli wa mambo uwe muhimu zaidi badala ya maslahi ya kisiasa, ubaguzi wa rangi, maoni ya upande mmoja wa itikadi, tushirikiane kujenga mazingira mazuri ya maoni ya watu wa kimataifa yanayotetea haki, kuongeza hamasa na kuleta matumaini .

Watu wenye nia moja hawawezi kutenganishwa kwa umbali. Katika mwaka uliopita, marafiki wa CMG waliongezeka. Sisi na wenzetu wa vyombo vya habari vya kimataifa, tulitumiana barua zaidi ya 600, kukutana ana kwa ana au kwa njia ya video zaidi ya mara 20. Tulishirikiana kuanzisha utaratibu wa ushirikiano wa kiwenzi wa vyombo vya habari wenye masikilizano, usawa na hali ya kuaminiana, mawasiliano mbalimbali yenye uwazi yamejenga daraja la kuaminika, barua mbalimbali za kusisimua zinatuhimiza kufanya kazi zetu vizuri zaidi. Tunawashukuru!

Katika zama hizi ambazo lolote linaweza kutokea, tunakabiliwa na mageuzi ya vyombo vya habari kwa mtazamo wa “ndovu angejua kucheza ngoma”. Katika Michezo ya Olimpiki ya Tokyo, CMG ilifaulu kurusha matangazo ya moja kwa moja ya mashindano kwa teknolojia ya 4K kwa mara ya kwanza duniani. Vipindi vyetu vya Michezo ya Olimpiki vilipata watazamaji zaidi ya milioni 400 miezi mitatu baada ya kuanzishwa . Na baada ya siku zaidi ya 30 wakati wa mwaka mpya wa jadi wa China, mwenge wa Olimpiki utawashwa tena hapa Beijing. Kupitia teknolojia ya “5G+4K/8K+AI”, CMG itaanza kutoa matangazo ya moja kwa moja katika behewa ya reli ya mwendo kasi kati ya Beijing na Zhangjiakou, hii itatatua swala gumu la kiteknolojia la kutangaza kwa njia ya video kwenye reli ya mwendo kasi kwa mara ya kwanza duniani. Tunakaribisha wenzetu wa nchi mbalimbali kutumia teknolojia hiyo, na kuionyesha dunia nzima Michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi ya Beijing.

Chui milia kuunguruma mlimani kunamaanisha ustawi wa taifa, upepo mwororo kutikisa miti kunaashiria majira ya mchipuko kuwadia. Katika mwaka mpya, Mkutano Mkuu wa 20 wa Chama cha Kikomunisti cha China utafanyika, ambao utapanga mpango mpya wa siku za baadaye za China. Sisi tutaendelea kuandaa vipindi vizuri kwa makini, kuchapa kazi ili kuonyesha kutoka pande mbalimbali uhai mkubwa wa China katika zama mpya , na kuviwezesha vyombo vya habari vitoe mchango kwa ajili ya kujenga jumuiya ya binadamu yenye mustakabali wa pamoja.

Nawatakia tena kila la heri , na baraka ya dunia!