Polisi nchini Somalia jana wamesema, watu 10 wameuawa wakiwemo wanajeshi watano na wengine 9 kujeruhiwa baada ya gari lilotegwa mabomu kulipuka karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa katika mji mkuu wa nchi hiyo, Mogadishu.
Polisi pia wamesema, shambulizi hilo lililenga msafara uliokuwa ukisindikiza wageni kwenye barabara kuu karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa, na uchunguzi unaendelea.
Habair zinasema, kundi la al-Shabaab nchini Somalia limekiri kuhusika na shambulizi hilo.