China na Afrika zinaungana mikono kuonyesha moyo wa mshikamano na kujiendeleza
2022-02-10 07:55:51| cri

China na Afrika zinaungana mikono kuonyesha moyo wa mshikamano na kujiendeleza_fororder_非盟 头图

Rais Xi Jinping wa China hivi karibuni aliutumia barua mkutano wa 35 wa wakuu wa Umoja wa Afrika, akipongeza moyo wa mshikamano na kujiendeleza ulioonyeshwa na nchi za Afrika chini ya uongozi wa Umoja wa Afrika, pamoja na juhudi zao zisizo na ukomo za kujitafutia njia za maendeleo zinazolingana na hali zao.

Huu ni mwaka wa 20 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Afrika na mwaka wa kwanza wa utekelezaji wa Mpango wa Dakar(2022-2024) uliofikiwa kwenye Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika. Katika miaka 20 iliyopita, uhusiano kati ya China na Afrika umeimarishwa zaidi, na ushawishi na hadhi ya nchi za Afrika kimataifa vimeendelea kuongezeka. Tukiwa tunadhani kwamba juhudi zetu kwa kiasi kikubwa zimeanzisha utaratibu mzuri zaidi wa kimataifa, mlipuko wa ghafla wa janga la COVID-19 umefichua vya kutosha hali ya ukosefu wa haki kwenye utaratibu huo, na watu wanaoathiriwa zaidi ni wa Afrika.

Takwimu zimeonesha kuwa mwaka jana bara la Afrika lilikumbwa na mdororo wake wa kwanza wa kiuchumi katika miongo kadhaa, huku shughuli za kiuchumi zikishuka kwa 2%. Mambo kama vile kupanda kwa mfumuko wa bei na kupanda kwa mizigo ya madeni yanazuia kufufuka kwa uchumi. Wakati huo huo, ni 10% tu ya watu wa Afrika wamepewa chanjo kamili dhidi ya Covid-19, huku kiwango hiki katika nchi tajiri kikiwa ni mara saba zaidi kuliko kile cha barani Afrika. Kama alivyosema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, "mfumo wa kifedha wa kimataifa uliofilisika kimaadili umezitelekeza nchi zinazoendelea".

Katika mkutano wa nane wa mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika uliofanyika Novemba mwaka jana, Xi Jinping alitangaza "miradi tisa" ya ushirikiano na Afrika katika miaka mitatu ijayo kuanzia mwaka huu. Kwa kuunganisha ujenzi wa pamoja wa ushirikiano wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja", "Pendekezo la Maendeleo ya Dunia" na "Ajenda 2063" ya Umoja wa Afrika kama nguzo kuu, kama nchi kubwa zaidi inayoendelea duniani na bara lenye nchi nyingi zaidi zinazoendelea, China na Afrika zinapaswa kuungana mikono zaidi na kujiendeleza, jambo ambalo ni muhimu na lenye nguvu zaidi kuliko hapo awali.

Kamishna wa Umoja wa Afrika anayeshughulikia mambo ya afya, ubinadamu na maendeleo ya Jamii Samate Cessouma Minata aliwaambia waandishi wa habari kando ya mkutano wa kilele wa AU kwamba China imekuwa ikisaidia AU na nchi wanachama wake kupambana na athari za janga hilo tangu kulipuka kwake. Mwishoni mwa mwaka jana, China ilitangaza kutoa dozi bilioni 1 za chanjo kwa Afrika, ambapo milioni 600 zitakuwa misaada ya bure. Wakati huo huo, Tume ya Umoja wa Afrika na wanachama wake wanafanya kazi ya kuwezesha kuzalisha chanjo ndani ya Afrika, na China imekuwa mshirika mkuu katika jitihada hizi. Minata alisema ushirikiano kati ya AU na China sio tu umeokoa maisha ya watu wa Afrika, lakini pia umehakikisha usalama wa chakula wa bara la Afrika.

China inajua sana kwamba ni kwa kudhibiti kuenea kwa janga hilo tu ndipo utaratibu wa kawaida wa kiuchumi na kijamii katika nchi za Afrika unaweza kurejeshwa. Kulingana na uchunguzi wa hivi karibuni kwa makampuni 1,116 ya China barani Afrika uliofanywa na Taasisi ya Asia Magharibi na Afrika ya Baraza la China la Kukuza Biashara ya Kimataifa, asilimia 48.36 ya makampuni yanayowekeza barani Afrika na 48.8% ya makampuni yanayofanya biashara barani Afrika yana mipango ya upanuzi. Hii inaonyesha kuwa fursa nyingi za uwekezaji barani Afrika na soko kubwa la wateja bado zinavutia sana makampuni ya China. Kwa kuangalia hali halisi barani Afrika, China inajitahidi kuunda njia ya kijani kwa ajili ya mauzo ya nje ya bidhaa za kilimo za Afrika, kupanua ushuru wa sifuri kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka Afrika, na kupanga kuagiza bidhaa zenye thamani ya dola bilioni 300 kutoka Afrika katika miaka mitatu ijayo. Wakati huo huo, China na Afrika zitapanua zaidi ujenzi wa maeneo ya kiviwanda ili kuona ni bidhaa gani, mashamba na huduma zipi zinafaa kwa mauzo ya nje kwenda China, jambo ambalo pia litasaidia katika maendeleo ya viwanda vya ndani barani Afrika.

Inaaminika kuwa maendeleo thabiti ya uhusiano kati ya China na Afrika yataonyesha dunia umuhimu wa uhusiano wa kiwenzi unaozingatia moyo wa mshikamano na kujiendeleza na unaozingatia ushirikiano wa kunufaishana. Ikiwa mwenyekiti mwenza wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika mwaka jana, Senegal ilichukua bendera ya urais mpya wa zamu wa AU katika mkutano wa mwaka huu wa AU. Bahati hii pia inaashiria kuwa China na Afrika zitaweza kufanikiwa kuboresha utaratibu wa kimataifa uwe wa haki zaidi na kujenga Afrika kuwa "chanzo cha matumaini" duniani.