Rais Xi Jinping ampongeza Bw. Steinmeier kwa kuchaguliwa tena kuwa Rais wa Ujerumani
2022-02-14 08:41:55| CRI

Rais Xi Jinping wa China amempongeza Bw. Frank-Walter Steinmeier kwa kuchaguliwa tena kuwa Rais wa Shirikisho la Ujerumani.

Kwenye salamu zake za pongezi Rais Xi amesema mwaka huu ni China na Ujerumani zinaadhimisha miaka 50 ya uhusiano wa kidiplomasia. Amesema China inathamini maendeleo ya ushirikiano kati ya China na Ujerumani, na iko tayari kufanya kazi pamoja na Bw. Steinmeier kuimarisha ushirikiano wa kimkakati wa pande zote kati ya pande hizo mbili, na kuufanya uhusiano kati ya pande hizo mbili ufikie kiwango kipya.