Watu 59 wamefariki na wengine 55 kujeruhiwa katika mlipuko wa mgodi wa dhahabu uliotokea jana huko Gbomblora, mkoa wa Poni, kusini magharibi mwa Burkina Faso.
Chanzo cha mlipuko huo bado hakijajulikana, lakini mashuhuda kadhaa walieleza kuwa mlipuko huo ulitokana na moto ambao uliteketeza vilipuzi vinavyotumiwa na wachimbaji dhahabu wakati wa shughuli zao.