Mawaziri wa mambo ya nje wa Algeria, Tanzania na Zambia watarajia kuzuru China
2022-03-18 08:09:17| cri

Mawaziri wa mambo ya nje wa Algeria, Tanzania na Zambia watarajia kuzuru China_fororder_赵立坚

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Zhao Lijian jana amesema, mawaziri wa mambo ya nje kutoka Tanzania, Algeria na Zambia wanatarajiwa kufanya ziara ya siku 4 nchini China kuanzia leo. Wakiwa nchini China, mawaziri hao watakutana na kufanya mazungumzo na mwenzao wa China, Wang Yi.