Kisiwa cha kuvutia cha Msumbiji kilichoandikwa kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia wa UNESCO
2023-01-12 12:35:12| cri

Mji wa Nampula uko kati ya Mfereji wa Msumbiji na Ghuba ya Mossuril, ambao ni mojawapo ya vivutio muhimu vya utalii nchini Msumbiji. Kama koloni la zamani la Ureno, Msumbiji ambako watu wanatumia lugha 40 tofauti, licha ya rasilimali nyingi, ni moja ya nchi masikini zaidi katika bara la Afrika. Kisiwa cha Msumbiji kiko kwenye orodha ya Urithi wa Dunia wa UNESCO kutokana na historia yake tajiri na fukwe.