Polisi 8 wa Kenya wauawa katika mlipuko unaoshukiwa kutekelezwa na Al-shabaab
2023-06-16 20:51:35| cri

Polisi nchini Kenya wamesema, askari polisi wanane wa Kenya wameuawa baada ya gari lao kushambuliwa kwa mabomu na watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa kundi la Al-shabaab.

Shambulio hilo limetokea katika kaunti ya Garissa, mashariki mwa Kenya, ambapo kundi la al-Shabaab limekuwa likifanya mashambulizi dhidi ya serikali ya Somalia kwa zaidi ya miaka 15.