Wakulima wa vitunguu nchini Kenya wanaendelea kuvuna pato la juu lililoongezeka kwa asilimia 650 tangu Februari.
Bei ya kilo moja ya kitunguu chekundu ilikuwa shilingi 20 mwezi wa Februari lakini kwa sasa ni Sh150. Bei hiyo imekuwa ikipanda ghafla nchini Kenya kutokana na uhaba mkubwa uliosababishwa na ukame na pia kujikokota kwa uagizaji kutoka nchi jirani ya Tanzania. Wakulima wanasema kwamba hiyo ndio bei ya juu zaidi ambayo inawapa faida kubwa. Aidha baadhi ya wakulima wanaona huenda wakavuna pakuwa ikiwa uagizaji kutoka Tanzania utaondolewe. Baada ya ukame kukumba maeneo mengi ya Kenya wakulima wengi wa kitunguu waliokuwa wameenda hasara kubwa katika msimu wa Oktoba hadi Desemba waliogopa kupanda. Hata hivyo, wakulima wengi wa Kenya wanalalamikia gharama kubwa ya uzalishaji.