Wanajeshi watano wauawa katika shambulizi la kigaidi nchini Mali
2023-09-20 08:40:41| CRI

Jeshi la Mali limesema, watu 45 wameuawa wakiwemo askari watano wa jeshi hilo na magaidi 40 katika shambulizi dhidi ya vikosi vya jeshi la Mali kaskazini mwa nchi hiyo.

Magaidi waliokuwa kwenye magari na pikipiki walivamia kambi za jeshi la nchi hiyo na mgambo zilizoko Lere, kaskazini mwa Mali, ambapo askari 40 walijeruhiwa na wengine 11 hawajulikani walipo.

Tangu mwaka 2012, Mali imekumbwa na mgogoro mkubwa wa kiusalama, kisiasa na kiuchumi. Uasi, uvamizi wa wapiganaji wa jihadi na vurugu za kikabila zimesababisha maelfu ya watu kuuawa na mamia ya maelfu ya watu kukimbia makazi yao.