Mashindano ya polo yafanyika mjini Nairobi, Kenya
2023-09-26 23:40:20| cri

Wachezaji wa mashindao ya polo walisalimiana kwa ngumi tarehe 23 baada ya mashindano ya Kombe la Casino yaliyofanyika kwenye klabu ya polo ya Nairobi, Kenya.

Klabu ya polo ya Nairobi ilianzishwa mwaka 1907, ikiwa na historia ndefu zaidi Afrika Mashariki, na inaandaa mashindano kadhaa maarufu kila mwaka. Mchezo wa polo kwa sasa unawavutia watu wengi zaidi mjini Nairobi.