Malawi kuwarejesha makwao zaidi ya wakimbizi 100 wa Burundi
2023-10-03 08:45:24| CRI

Zaidi ya wakimbizi 100 wa Burundi wanaoishi Malawi wanatazamiwa kurejea nyumbani Alhamisi, kufuatia mazungumzo kati ya serikali ya Malawi, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) na serikali ya Burundi.

Msemaji wa Wizara ya Usalama wa Ndani ya Malawi, Patrick Botha, alithibitisha tukio hilo kwa vyombo vya habari vya ndani Jumatatu, akisema wakimbizi 108 wanaoishi Dzaleka, kambi ya wakimbizi iliyoteuliwa na UNHCR nchini Malawi, walijitolea kurejea nyumbani.

Botha alisema zoezi la kuwarejesha lilitakiwa kufanyika Septemba 15, lakini lilisogezwa mbele hadi Oktoba 5 kutokana na matatizo ya maandalizi ya vifaa yaliyokabili zoezi hilo.

Kundi la kwanza la wakimbizi waliorejeshwa makwao kwa hiari liliondoka katika Kambi ya Dzaleka na kwenda katika nchi zao tofauti mwezi Juni kufuatia kampeni ya serikali ya Malawi ya kurudi kambini, ambayo Waziri wa Usalama wa Ndani Ken Zikhale Ng'oma aliianzisha ili kuwalazimisha wakimbizi wote wanaoishi nje ya Dzaleka kurejea kwenye kambi.