Matapeli watumia Akili Bandia kujifanya mkuu wa Umoja wa Afrika Moussa Faki
2023-10-19 23:03:10| cri

Tume ya Umoja wa Afrika imekuwa muhanga wa uhalifu wa mtandaoni baada ya matapeli kusambaza zana za kijasusi za akili bandia ili kumuiga mkuu wa tume hiyo Moussa Faki.

Huu unaweza kuwa upungufu wa kwanza wa kidiplomasia wa teknolojia mpya.

Bw Faki ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika, sekretarieti ya Umoja wa Afrika mara kwa mara huwaandikia viongozi wa kimataifa wakati wowote anapohitaji kupiga simu.

Barua kama hiyo inajulikana rasmi kama maelezo ya maneno na ni utaratibu wa kawaida wa kuratibu mikutano kati ya uongozi wa Umoja wa Afrika na wawakilishi wa nchi nyingine au mashirika ya kimataifa. Lakini matapeli walifeki sauti yake na kupiga simu kadhaa za video katika miji mikuu ya Ulaya, wakilenga kupanga mikutano.

Bado haijabainika matapeli hao walikuwa na nia gani, lakini taarifa ya AU ilisema barua pepe zao ni za uwongo, jambo linaloashiria kwamba wanaweza kuwa na nia ya kuiba vitambulisho vya kidijitali ili kupata taarifa muhimu.