Marekani yaiondoa Uganda kwenye mpango wa AGOA
2023-11-03 14:19:54| cri

RAIS wa Marekani Joe Biden amesema nchi za Uganda, Gabon, Niger na Jamhuri ya Afrika ya Kati zitatolewa kwenye mpango maalum wa kibiashara wa Marekani na Afrika unaojulikana kama AGOA.

Nchi hizo zimeondolewa kwenye mpango huo kutokana na kuhusika ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu au kutopiga hatua kuelekea utawala wa kidemokrasia, rais alisema. Marekani ilianzisha Sheria ya Ukuaji na Fursa Afrika (Agoa) mwaka 2000. 

Chini ya mpango huo, nchi zinazostahiki za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na ufikiaji bila ushuru wa Marekani kwa zaidi ya bidhaa 1,800. Rais Biden alisema kuwa Niger na Gabon zote mbili kwa sasa ziko chini ya utawala wa kijeshi kufuatia mapinduzi yaliyofanywa mwaka huu. 

Rais huyo alisema nchi hizo hazistahiki kuwepo kwenye mpango wa AGOA kwa sababu hazijaanzisha au hazifanyi maendeleo endelevu katika kuanzisha ulinzi wa vyama vingi vya kisiasa na utawala wa sheria.