Watu 110 wafariki nchini Somalia kufuatia mvua za El Nino
2023-12-05 10:59:53| cri

Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imesema, idadi ya vifo kutokana na mafuriko yanayoendelea nchini Somalia imeongezeka hadi 110, huku zaidi ya watu milioni moja wakikosa makazi.

Katika taarifa yake iliyotolewa jumapili, Ofisi hiyo pia imetoa tahadhari ya kutokea kwa magonjwa ya mlipuko kufuatia ripoti za kesi za watu wanaoshukiwa kuugua kipindupindu katika majimbo ya Hirshabelle na Galmudug.

OCHA imesema, boti 37 zimepelekwa kupeleka vifaa au kuwahamisha wale waliokwama na maji ya mafuriko.