Idadi ya vifo vya Wapalestina huko Gaza yaongezeka hadi 20,674
2023-12-26 09:24:33| CRI

Wizara ya Afya yenye makao yake Gaza imetangaza kuwa takriban Wapalestina 20,674 wameuawa, na wengine 54,536 kujeruhiwa katika mzozo unaoendelea kati ya Israel na Hamas  tokea Oktoba 7.

Wizara hiyo Jumatatu ilisema katika muda wa saa 24 zilizopita, Wapalestina 250 walikufa katika mashambaulizi 25  kutoka anga na ardhini  yaliyofanywa na vikosi vya Israel  dhidi ya eneo lote.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina iliilaani Israel kwa kupuuza wito wa kimataifa wa kusitishwa kwa mashambulizi ya kijeshi dhidi ya raia wa Palestina na kuwazuia wanamgambo walowezi.

Wakati huo huo, wizara hiyo imesisitiza haja ya kupitishwa azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa la kusitisha mapigano ili kuruhusu utolewaji wa  msaada ulio salama na wa haraka na kuhakikisha usalama wa raia wa Palestina.