Mashirika ya ndege ya Afrika yaadhimisha mwaka wa nne salama wa safari za ndege
2024-03-06 13:42:32| cri

Mashirika ya ndege ya Afrika yamerekodi mwaka wa nne mfululizo wa kutokuwa na ajali kubwa.

Kwa mujibu wa tathmini ya usalama wa ndege wa Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (IATA) ya mwaka 2023, mashirika ya ndege ya Afrika hayajapata hasara hata moja ya ndege ya abiria au ajali mbaya tangu 2020. Mwaka jana pia ilikuwa mara ya tano kwa Afrika kutokuwa na ajali kubwa zilizohusisha ndege za mapangaboi katika miaka tisa iliyopita.