Watu 91 walifariki katika ajali ya meli kaskazini mwa Msumbiji
2024-04-08 08:48:19| cri

Watu 91 wamefariki na wengine 34 hawajulikani walipo baada ya meli waliyopanda kupata ajali karibu na Kisiwa cha Msumbiji katika Mkoa wa Nampula kaskazini mwa Msumbiji siku ya Jumapili.

Mkuu wa mkoa wa Nampula, Jaime Neto amesema meli hiyo ilikuwa inatumika kama kivuko cha muda kutoka eneo la Mossuril mkoani humo, na ilikuwa na abiria 130 wakati ajali hiyo ikitokea, na kuongeza kuwa, huenda chanzo cha ajali hiyo ni mzigo mkubwa.

Bw. Neto amesema mpaka sasa watu watano wameokolewa, na wawili kati yao wamepelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu.