UDSM chapanua wigo wake kimataifa kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Hunan
2024-05-08 13:35:25| cri

Mkakati wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kupanua wigo wake kimataifa kupitia mashirikiano mbalimbali na vyuo vikuu vya nje umeendelea kuzaa matunda.

Chuo kikuu hiki kimesaini Makubaliano ya Maelewano (MoU) na Chuo Kikuu cha Hunan cha China. Makubaliano hayo, yaliyosainiwa Jumatatu, Mei 6, 2024, UDSM, yaliashiria kuanza kwa ushirikiano wa kimkakati kati ya taasisi hizi maarufu na kupiga hatua kubwa katika kukuza ushirikiano wa kimataifa katika elimu na utafiti.

Kwenye ushirikiano huu, vyuo vikuu viwili vimekubaliana kuongeza mawasiliano ya kitaaluma, ushirikiano wa utafiti, na uelewa wa kitamaduni, ambayo ni msingi wa ushirikiano kati ya vyuo vikuu kutoka nchi mbalimbali.