Treni ya abiria ya TAZARA kuanza kutoa huduma baada ya kusimamishwa kwa siku 50
2024-05-23 23:14:09| cri

Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) imetangaza kurejesha safari za treni katika maeneo tofauti ikiwemo njia ya Dar es Salaam-Kapiri Mposhi.

Kusimamishwa kwa huduma kuliathiri vibaya usafirishaji huru wa bidhaa kati ya Tanzania na Zambia ambazo zimekuwa zikishirikiana kihistoria katika biashara, na kusababisha hasara kwa wahusika wengi.

Akitangaza kurejea kwa shughuli za kawaida za treni, Mkuu wa Masuala ya Umma wa mamlaka hiyo, Bw. Conrad Simuchile, amesema shughuli katika njia kuu zilisitishwa kutokana na maporomoko ya udongo kufuatia mvua kubwa iliyonyesha katika maeneo mbalimbali ya Tanzania, hasa katika eneo la Mlimba-Makambako nchini Tanzania.