Watu 4 wafa maji na wengine watatu hawajulikani walipo baada ya mashua kuzama kusini mwa Tanzania
2024-05-27 09:20:16| CRI

Afisa wa Tanzania jana usiku alisema kuwa wakulima wanne wamekufa maji na wengine watatu hawajulikani walipo baada ya mashua yao kuzama mtoni katika mkoa wa Katavi kusini mwa Tanzania.

Mkuu wa mkoa wa Katavi Bi. Mwanamvua Mrindoko alisema ajali hiyo ilitokea Ijumaa usiku wakati mashua hiyo ambayo ilibeba magunia 10 ya mpunga, ilipozama katika mto Ukingwamizi wilaya ya Mlele. Watu saba waliogelea hadi eneo salama.

Waokoaji, wakiongozwa na Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji Tanzania, walipata mwili wa mkulima mmoja siku ya Jumamosi, na miili mingine mitatu iliopolewa Jumapili. Amefafanua kuwa waokoaji wanaendelea kuwasaka wakulima watatu ambao hawajapatikana na kuongeza kuwa mto huo ulikuwa umejaa maji kutokana na mvua kubwa iliyoendelea kunyesha mwezi uliopita.