Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania yazindua kampeni nchi nzima ya kuanzisha klabu za kidijitali mashuleni
2024-06-11 10:52:50| cri

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezindua kampeni nchi nzima ya kuhimiza uanzishwaji wa klabu za kidijitali mashuleni kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu. Mpango huu ni sehemu ya mkakati wa kupanua ufikikaji wa tehama na matumizi ya teknolojia za kidijitali. Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dk Jabiri Bakari amesema mpango huo unatekelezwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu na TEHAMA, ili kuhakikisha uanzishwaji wa klabu za kidijitali katika kila ngazi ya elimu. Amesema vilabu vya dijitali ni msingi muhimu wa ubunifu wa nyumbani na ubunifu katika kupunguza changamoto za nyumbani. Ameongeza kuwa kampeni itatekelezwa katika maeneo ya Zanzibar, nyanda za juu kusini, kati, kaskazini, mashariki, na kanda ya ziwa.