Safari ya utalii isiyosahaulika nchini Tanzania ya wanandoa wazee kutoka Afrika Kusini
2024-06-19 14:02:15| cri

Lyn Bach na mumewe wana umri wa miaka 70 na miaka 75, mtawaliwa. Wamerejea nyumbani Afrika Kusini baada ya wiki moja ya kuwinda na wawindaji wa Kihadzabe, wakichuma buni kutoka kwenye mti, na kuangalia karamu ya chui aliyetoka kuchinjwa.

Katika muda usiozidi siku saba nchini Tanzania, walikuwa wakistaajabishwa na uzuri wa utulivu wa nchi na watu wake. Lyn na mume wake walimkabidhi kiongozi wa eneo hilo kuandaa shughuli na maeneo yote ya kutembelea, na walishangaa sana kuona kwamba ziara yao ilizidi matarajio yao ya awali.

"Kusema kweli, kila mahali tulipogeuka palikuwa pazuri kushinda pengine," Lyn alisema kwa furaha.

Lyn alisikia habari kuhusu Tanzania kutoka kwa mhadhiri mashuhuri anayependa kusafiri Bw Moshe, miaka 10 iliyopita. Na wakati ulipowadia, waliamua kwamba maneno pekee hayatoshi kukata kiu yao, na kulazimika kujionea wenyewe nchi ambayo kila mtu anaizungumzia kwa furaha sana.