WHO yasema Tanzania yapiga hatua kubwa kiafya
2024-06-28 08:58:06| CRI

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeipongeza Tanzania kwa kupiga hatua kubwa katika hali yake ya afya.

Katika Ripoti ya kila miaka miwili ya WHO Tanzania 2022-2023 iliyotolewa Alhamisi, ambayo imeorodhesha mafanikio kadhaa katika sekta ya afya ya Tanzania, ikiwemo kupungua kwa kiwango cha vifo vya uzazi, shirika hilo lilisema kuwa na watu wenye afya nzuri ni muhimu kwa ustawi wa uchumi wa Tanzania. Inabainisha kuwa vifo vinavyotokana na ujauzito vilipungua kwa kasi kutoka 556 kwa kila watoto 100,000 waliozaliwa wakiwa hai mwaka 2015 hadi 104 mwaka 2022.

Kwa mujibu wa ripoti, Tanzania ilipiga hatua kubwa katika kuongeza upatikanaji wa chanjo kutoka chini ya asilimia 2.8 mwaka 2021 hadi asilimia 53.8 mwaka 2023 kwa kutumia juhudi zinazoungwa mkono na WHO. Mafanikio mengine makubwa ni kwamba bunge la Tanzania lilipitisha Mswada wa Bima ya Afya kwa Wote, ukiwezeshwa na mwongozo wa kitaalamu na mapitio kutoka WHO na washirika wake.