Rais wa China kuhudhuria Mkutano wa SCO na kufanya ziara katika Kazakhstan na Tajikistan
2024-06-30 17:46:11| CRI

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Bibi Hua Chunying ametangaza kuwa, kuanzia tarehe 2 hadi 6 mwezi Julai, rais Xi Jinping wa China atahudhuria Mkutano wa 24 wa Baraza la Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai (SCO) utakaofanyika huko Astana, na kufanya ziara ya kiserikali katika nchi za Kazakhstan na Tajikistan kwa kufuata mialiko ya marais wa nchi hizo mbili.