Sudan na Iran zatumiana mabalozi wakati hali ya kidiplomasia kati yao ikiboreka
2024-07-22 14:46:58| cri

Wakati uhusiano kati ya Sudan na Iran ukipata maendeleo muhimu wa kuelekea kuwa wa kawaida, mwenyekiti wa Baraza la Mpito la Sudan Abdel Fattah al-Burhan amepokea rasmi hati za utambulisho za balozi mpya wa Iran Hassan Shah Hosseini, huko Port Sudan.

Katika taarifa yake baraza hilo limetaja hatua hiyo kama mwanzo wa awamu mpya ya uhusiano wa pande mbili kati ya nchi hizo. Naibu Katibu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan Hussein al-Amin amesisitiza kuwa mabadilishano ya mabalozi ni sehemu muhimu ya kuendeleza ushirikiano.

Mjumbe huyo wa Iran ameeleza dhamira yake ya kuimarisha uhusiano, na akisisitiza dhamira ya pande zote ya kuimarisha uhusiano. Siku hiyo balozi mpya wa Sudan nchini Iran Abdulaziz Hassan Saleh aliondoka kuelekea Tehran na anatarajiwa kuanza kazi hivi karibuni.