Tanzania kuwa mwenyeji wa luteka ya pamoja na China katika kuadhimisha miaka 60 ya uhusiano wa nchi hizo mbili
2024-07-25 11:07:30| cri

Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa luteka ya kijeshi na China baadaye wiki hii, kufuatia kuwasili kwa meli tatu za wanamaji za wanajeshi wa China. Luteka hiyo itafanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 60 ya uhusiano kati ya nchi hizo mbili na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Wanajeshi wa China watashiriki kwenye mafunzo ya pamoja na JWTZ, yakijumuisha operesheni mbalimbali za kijeshi, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya majeshi ya nchi hizo mbili.

Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Tanzania, Ameir Ramadhan Hassan, ameeleza matumaini yake kuhusu luteka hiyo, akionyesha fursa ya kubadilishana ujuzi na uzoefu kati ya wanajeshi nchi hizo mbili. Amesema wanatarajia kuwa luteka hiyo itaimarisha uwezo wa kijeshi wa Tanzania na kukuza uhusiano wa karibu na Jeshi la Ukombozi wa Umma la China.