Tanzania yaeleza sababu za kucheleweshwa kuidhinisha eneo la biashara huria la jumuiya tatu
2024-07-26 23:13:10| cri

Serikali ya Tanzania imeeleza sababu ya kuchelewa kuridhia mkataba wa kibiashara wa kikanda ulioanza kufanya kazi mwaka jana, ikisema inakamilisha taratibu za kisheria za ndani.

Makubaliano ya Eneo Huru la Biashara la jumuiya tatu za kiuchumi (TFTA) ya COMESA-EAC-SADC yalianza kufanya kazi Julai 25, 2024, huku nchi 14 kati ya 29 wanachama zikiidhinisha.

Jumatano Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ilitangaza kwamba makubaliano hayo yataanza kutumika kufuatia kufikiwa kwa kiwango kinachohitajika cha nchi 14 wanachama. Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo bado hazijakabidhi hati zao za kuridhia, huku serikali ikisema juhudi zinafanywa ili kukamilisha mchakato wa serikali kuridhia mkataba huo mapema iwezekanavyo.