Kenya, Uganda zafichua mtandao wa bidhaa haramu za matibabu
2024-07-26 14:13:50| cri

Bodi ya Famasia na Sumu ya Kenya (PPB) na Mamlaka ya Taifa ya Dawa za Uganda, zimefichua mtandao unaosumbua wa bidhaa haramu za matibabu zinazosafirishwa katika nchi zote mbili kupitia njia za posta na anga. Bidhaa zilizokamatwa, ambazo ni pamoja na dawa za binadamu, bidhaa za kibiolojia na virutubisho vya lishe, zinahatarisha afya ya umma na kuangazia changamoto inayokua ya kudhibiti biashara ya dawa za kuvuka mipaka.

Katika operesheni hiyo, timu hiyo ilipata dawa zilizokuwa zimehifadhiwa na kusafirishwa nje ya masharti yaliyoidhinishwa; dawa zisizo na oda halali na ambazo hazijatangazwa ili kuepusha kugunduliwa; na virutubisho vya lishe vinavyojulikana kuwa na viambato vya dawa ambavyo havijatangazwa vilivyoingizwa nchini kinyume na kanuni. Timu ya utekelezaji iliyohusika katika kufichua mtandao huo ilijumuisha mashirika kutoka Kenya na Uganda, Marekani, Uingereza, na Umoja wa Ulaya, pamoja na mashirika ya kimataifa na sekta ya dawa.