Mkutano wa kilele wa FOCAC wafunguliwa Beijing
2024-09-05 12:31:35| cri

Mkutano wa kilele wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC umefunguliwa leo tarehe 5 hapa Beijing, ambapo rais Xi Jinping alitoa hotuba akitangaza kuinua uhusiano kati ya China na nchi zote za Afrika zenye uhusiano wa kibalozi kwenye ngazi ya kimkakati, na uhusiano kati ya China na Afrika kwa ujumla ufikie kwenye jumuiya yenye mustakabali wa pamoja ya hali zote katika zama mpya.

Rais Xi amesema katika miaka 24 iliyopita tangu kuanzishwa kwa FOCAC mwaka 2000, China na nchi za Afrika zimeelewana na kuungana mkono, na kutoa mfano wa kuigwa kwa uhusiano wa kimataifa wa aina mpya.

Ameeleza kuwa China na Afrika zinachukua theluthi moja ya watu wote duniani, hivyo bila ya China na Afrika kuwa ya mambo kisasa, hakutakuwa na dunia ya mambo ya kisasa. Katika miaka mitatu ijayo, China inapenda kushirikiana na Afrika kutekeleza mipango 10 ya kuendeleza mambo ya kisasa kupitia ushirikiano wa kukuza kufunzana kuhusu ustaarabu wa kisasa, ustawi wa biashara, mlolongo wa viwanda, mafungamano ya mawasiliano, maendeleo, afya, kilimo, mawasiliano ya watu, nishati za kijani na usalama ili kuimarisha ushirikiano kati ya China na Afrika na kuongoza mambo ya kisasa ya nchi za Kusini.

Amebainisha kuwa, nchi za Afrika zinasukuma mbele lengo lake la kutimiza mambo ya kisasa la Ajenda ya mwaka 2063. Na China na Afrika kutaka kutimiza ndoto zao za mambo ya kisasa kwa pamoja, hakika kutaanzisha wimbi la mambo ya kisasa la nchi za Kusini, na kufungua ukurasa mpya wa kujenga jumuiya ya binadamu yenye mustakabali wa pamoja. 

Ameongeza kuwa, China na Afrika zinapaswa kushirikiana kutimiza mambo ya kisasa katika pande sita, yaani kushirikiana kuhimiza mambo ya kisasa yenye haki na usawa, kushirikiana kuhimiza mambo ya kisasa yenye uwazi na kunufaishana, kushirikiana kuhimiza mambo ya kisasa yanayotoa kipaumbele maslahi ya wananchi, kushirikiana kuhimiza mambo ya kisasa yenye ujumuishi, na kushirikiana kuhimiza mambo ya kisasa yanayosaidia uhifadhi wa mazingira, pamoja na kushirikiana kuhimiza mambo ya kisasa yenye amani na usalama.