Wataalamu wakutana Kenya kujadili mikakati ya kukabiliana na hali ya hewa kwa miundombinu thabiti
2024-10-29 10:08:05| CRI

Wataalamu wa mabadiliko ya tabianchi Jumatatu walianza mkutano wa siku nne mjini Nairobi, nchini Kenya, kujadili mikakati ya kuongeza mahitaji ya kukabiliana na hali ya hewa kwa ajili ya miundombinu thabiti.

Mkutano huo uliopewa jina la “Shule ya Kurekebisha Mabadiliko ya Tabianchi”, na kuandaliwa na Chuo Kikuu cha Nairobi (UoN) na Kituo cha Kimataifa cha Kurekebisha (GCA), uliwaleta pamoja wataalam 50 wakati ambapo mabadiliko ya tabianchi yanaendelea kutishia mifumo ya miundombinu. Washiriki watachunguza namna ya kufanya tathmini za hatari ya hali ya hewa, kutambua udhaifu, na kubuni mikakati ya kukabiliana na hali ya hewa ili kuimarisha uthabiti wa miundombinu.

Mkurugenzi wa kanda ya Afrika katika GCA, Charles Nhemachena, alisema ulinzi wa kijamii na kiuchumi unaohusishwa na mabadiliko ya hali ya hewa husababisha uharibifu wa gharama kubwa, ukarabati na matengenezo katika nchi nyingi.

Naye mwenyekiti wa Idara ya Ardhi na Sayansi ya Hali ya Hewa katika Chuo Kikuu cha Nairobi, Daniel Olago, alisema kuwa mkutano huo umeazimia kuchukua hatua inayokusudiwa kuziba pengo kati ya sayansi, sera, na utekelezaji wa vitendo.