• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Novemba 12-Novemba 18)

    (GMT+08:00) 2016-11-18 18:38:21

    Pombe Magufuli, atia saini sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016

    Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli, hatimaye ametia saini sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016, sheria ambayo ilipitishwa wakati wa kikao cha bunge la 11 mjini Dodoma.

    Sheria hiyo iliyopitishwa na Bunge la Tanzania Jumamosi 5 Novemba mjini Dodoma.

    Kutiwa saini kwa sheria hii, kunatamatisha safari ndefu ya mijadala na maoni kuhusu maboresho ya muswada huo, ambapo majuma kadhaa yaliyopita wakati akizungumza na wahariri kwenye ikulu ya Dar es Salaam, Rais Magufuli aliapa kutia saini sheria hiyo punde tu ikifika mezani kwake.

    Punde baada ya kutia saini muswada huo wa huduma za habari kuwa sheria, rais Magufuli akawapongeza wadau wote walioshiriki kutoa maoni yao kuhusu kuboreshwa kwa muswada wenyewe ambapo wabunge waliupitisha kwa kauli moja mjini Dodoma.


    1 2 3 4 5 6 7 8
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako