Watu saba wakamatwa kwa kupanga kushambulia vituo vya polisi na mahali pa umma nchini Ufaransa
Watu saba wamewekwa kizuizini nchini Ufaransa wiki hii kutokana na kupanga kufanya mashambulizi dhidi ya vituo vya polisi na bustani ya umma nchini Ufaransa.
Mtuhumiwa mmoja amesema walipanga kushambulia vituo vya polisi kusini na mashariki mwa Ufaransa. Wanamue wawili walikamatwa wikiendi iliyopita mjini Marseille, na watuhumiwa wengine wanne wamekamatwa mjini Strasbourg, ambako duka kubwa kabisa kwa ajili ya sikukuu ya Krismas linatarajiwa kufunguliwa.
Watuhumiwa hao saba wanatoka Ufaransa, Morocco na Afghanistan. Hadi sasa watu 418 wamekamatwa nchini humo kufuatia operesheni za usalama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |