• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Disemba 10-16)

    (GMT+08:00) 2016-12-16 18:43:15

    Zika yagunduliwa Tanzania

    Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu, nchini Tanzania NIMR inasema imethibitisha kugunduliwa kwa virusi vya Zika nchini humo.

    Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Dkt Mwele Malecela, anasema wiki hii kwamba virusi hivyo vimepatikana mkoani Morogoro, Mashariki mwa Tanzania na Mkoani Geita, kaskazini magharibi mwa Tanzania.

    Utafiti huo ulifanyika kutokana na uhalisia kuwa kuna mazingira yanayowezesha kuzaliana kwa mbu wanaoeneza virusi hivyo.

    Dkt Mwele Malecela amesema kwamba kwa sasa serikali inaangazia kuzuia wajawazito wasiumwe na mbu ambao wanaaminika kueneza virusi hivyo.

    Hata hibvyo anasema bado wanajaribu kuangalia ni aina gani ya virusi vya Zika.

    Virusi vya Zika zimekuwa vikisababisha watoto kuzaliwa wakiwa na ubongo uliodumaa na vichwa vidogo katika mataifa ya Amerika Kusini na sana Brazil.


    1 2 3 4 5 6 7 8 9
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako