• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Disemba 10-16)

    (GMT+08:00) 2016-12-16 18:43:15

    Watu watatu wajeruhiwa baada ya gari lililotegwa bomu kulipuka nchini Somalia

    Gari lililotegwa bomu limelipuka kwenye mgahawa mmoja ulio karibu na ikulu ya mjini Mogadishu, Somalia, na kusababisha kifo cha mshambuliaji na watu wengine watatu kujeruhiwa.

    Msemaji wa manispaa ya Mogadishu Abdifitah Omar Halame amesema, lengo la mshambuliaji huyo lilikuwa ni kuua watu wengi zaidi, lakini hakufanikiwa kutokana na juhudi zilizofanywa na vikosi vya usalama vya nchi hiyo.

    Hakuna kundi lililokiri kuhusika na shambulizi hilo, lakini kundi la Al Shabaab limekuwa likifanya mashambulizi ya mara kwa mara nchini humo dhidi ya serikali.

    Hali ya usalama imeimarishwa mjini Mogadishu kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa rais tarehe 28 mwezi huu.


    1 2 3 4 5 6 7 8 9
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako