• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Januari 7-Januari13)

    (GMT+08:00) 2017-01-13 18:26:42

    Mohamed Osman Jawari achaguliwa tena kuwa spika wa bunge la Somalia

    Mohamed Osman Jawari amechaguliwa tena kuwa spika wa bunge la Somalia.

    Uchaguzi huo ulifanyika katika majengo ya Bunge mjini Mogadishu siku ya Jumatano, chini ya ulinzi mkali wa vikosi vya kulinda amani kutoka Umoja wa Afrika AMISOM.

    Kati ya wabunge 259 waliopiga kura, wabunge 141 walimchagua Jawari kuendelea kuongoza bunge kwa mara nyingine.

    Kuchaguliwa kwa spika huyu mwenye umri wa miaka 71 kutoka koo ya Digil na Mirifile, kunamaanisha kuwa mwanasiasa Sharif Hassan Sheikh Adan, ambaye anatoka naye katika koo hiyo atajiondoa katika orodha ya kuwania urais.

    Miongoni mwa wale wanaowania urais ni pamoja na rais wa sasa Hassan Sheikh Mohamud, rais wa zamani Sharif Sheikh Ahmed, Waziri Mkuu wa sasa Omar Abdirashid Ali Shamarke, na Waziri Mkuu wa zamani Mohamed Abdullahi Mohamed 'Farmajo'.


    1 2 3 4 5 6 7 8
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako